Waziri wa Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa, Wabunge waongoza wageni kushuhudia
msafara wa nyumbu ambao ni tukio kubwa duniani linalojulikana kwa lugha ya
Kingereza kama Serengeti Grand Migration na #NiSerengetiTena.
Katika tukio hilo la kwanza na la aina yake lililofanyika
kwenye eneo la Kogatende, Serengeti, wageni mbalimbali kutoka mataifa mengi
waliungana na viongozi hao wakishuhudia kwa zaidi ya saa 2 wanyama aina ya
nyumbu wakisindikizwa na pundamilia wakivuka na kupitia majaribu mbalimbali
ikiwemo kukabiliana na mamba kwenye Mto Mara.
Pamoja na Waziri wa Utalii Mhe. Mohammed Mchengerwa, Naibu
wake, Mary Masanja, Katibu Mkuu, Dkt. Hassan Abbasi na Naibu Katibu Mkuu
Benedict Wakulyamba, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na
Utalii, Mhe Timotheo Mnzava aliongoza baadhi ya wajumbe wa Kamati hizo
kushuhudia tukio hilo la kihistoria na kubaki wakishangazwa na maajabu hayo.
“Ndio tumeanza kutekeleza mikakati kabambe ya kuutangaza
utalii wetu. tukio hili ni la kihistoria na huwezi kulikuta popote duniani;
ujio wetu hapa ni kukipa heshima na kulitangaza zaidi duniani,” alisema Waziri
Mchengerwa.
“Tumejionea maajabu leo na tunaipongeza Serikali na
wahifadhi wetu kwa kuwalinda wanyama hawa mpaka leo tumejionea tukio hili la
aina yake,” alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii
Mhe. Mnzava.
Waziri wa Utalii Mhe. Mohammed Mchengerwa aliyesimama akitumia kionambali kuangalia msafara mkubwa wa nyumbu wanyama aina ya nyumbu wakisindikizwa na pundamilia wakivuka na kupitia majaribu mbalimbali ikiwemo kukabiliana na mamba kwenye Mto Mara.
0 Maoni