Vijana msimezwe na mitandao ya kijamii: DC Rufiji

 

Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Luteni Kanali Frederick Faustine Komba ametoa wito kwa vijana waliohitimu mafunzo ya kwa mujibu wa sheria Operesheni Nishati Safi 2025 kutomezwa na mitandao ya kijamii kwa sababu imekua chanzo cha kupoteza maadili .

DC Rufiji  Luteni Kanali Komba amesema hayo wakati alipokua mgeni rasmi kwenye sherehe za kufunga  mafunzo ya Oparesheni Nishati Safi  katika Kikosi 830 Kibiti  Mkoani Pwani.

"Zamani kulikua na sherehe  za jando kwa wanaume na unyago  kwa mabinti ambao walifindwa namna ya kuishi vizuri katika jamii hivyo basi mafunzo haya kwa vijana yanayotolewa  na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT)  yamebeba maudhui hayohayo ya kuwafundisha  vijana namna ya kuishi vema katika jamii.

Akifunga mafunzo hayo ya Operesheni Nishati  Safi Luteni Kanali Komba ametoa pongezi kwa Mkuu wa Kikosi cha Kibiti  830  Mohammed Karuma  pamoja na wakufunzi wote kutokana na mafunzo waliyoyatoa kwa vijana hao.

"Natoa pongezi zangu za dhati kwa Mkuu wa Kikosi  Kanali Mohammed Karuma pamoja na wakufunzi wote  kwa ujumla kutokana na mafunzo waliyoyatoa kwa vijana hawa ambao wametoka katika Mikoa mbalimbali  mbalimbali nchini mwetu huku wote wamekua wamoja" amesema Mkuu wa Wilaya ya Kibiti Luteni Kanali Komba.

Amesema kuwa weledi wa wakufunzi hao umewabadilisha vijana hao na kuwa wamoja na kuwasisitiza wahitimu hao waende kuishi waliyofundishwa.

"Nendeni mkawe mabalozi wazuri wa mafunzo ya JKT  huko muendako mkawe wawakilishi wema  pia mtambue kwamba maisha siyo rahisi mkajitunze na kuwa timamu kitabia na  kiafya sababu ninyi ndiyo viongozi wa taifa letu  kesho" amesema DC Rufiji  Luteni Kanali Komba.

Wakati huo huo amewataka vijana waliohitimu Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT kwa  Mujibu wa sheria 2025 kulinda kiapo chao na kutenda yale waliyofundishwa pindi watakaporejea nyumbani.

Yamesemwa hayo  na  aliyekuwa mgeni rasmi  katika kufunga mafunzo kwenye sherehe iliyifanyika   tarehe 18 Septemba 2025,yanayofahamika kama  Operesheni Nishati safi katika kikosi  830  Kibiti kilichopo Mkoani  Pwani.

Naye Mkurugenzi Rasilimali Watu Makao Makuu ya Jeshi Brigedia Jenerali Simon Pigapiga kwa Niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Jacob Mkunda amewataka vijana wanaohitimu mafunzo hayo kutumia kwa faida ujuzi waliyo upata katika kipindi chote cha mafunzo yao.

Aidha, Kanali Aranyael Nnko ambaye ni mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele amesema mafunzo hayo yamefanyika kwa kipindi cha  majuma kumi na Mawili yakijumuisha mafunzo ya awali ya kijeshi,  Kazi za mikono na uzalishaji Mali.

Wakati huohuo ametoa shukrani kwa wazazi waliotoa fursa kwa vijana wao kuhudhuria  mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa mujibu wa sheria 2025 ambayo kimsingi yanamjengea Kijana Uzalendo na Moyo wa Kupenda kazi.

"JKT ni mahali sahihi  na salama hivyo jamii na wazazi  msisite kuleta vijana wenu kuja kupata nafasi hii ambayo huwasaidia kuwajenga kizalendo na kuwapa mafunzo ya awali ya ulinzi na usalama pia ni haki kwa vijana wa kitanzania katika Kufundishwa Uzalendo na siyo vinginevyo" amesema Luteni Kanali Komba.




Chapisha Maoni

0 Maoni