Donald Trump amesema anapanga kujisalimisha Mahakamani siku
ya Alhamisi katika jimbo la Georgia kukabiliana na mashtaka ya kuingilia
uchaguzi.
Jaji wa Mahakama ya Atlanta anayesimamia kesi ya rais huyo
wa zamani wa Marekani, amempangia kulipa dhamana ya dola 200,000 za Marekani.
Makubaliano ya kesi hiyo yanasema kwamba Trump ataendelea
kuwa huru, iwapo tu hatojaribu kuwatisha mashahidi wa kesi hiyo.
0 Maoni