Jeshi la Uhifadhi lasisitizwa kuzingatia nidhamu na uadilifu

 

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba amesisitiza nidhamu katika kutekeleza majukumu ya kila siku na uadilifu katika kutunza na kulinda rasilimali za maliasili.

Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo Agosti 19, 2023, wakati akiongea na watumishi wa TAWA- Kanda ya Kati sambamba na kukagua miradi iliyotekelezwa kwa kupitia fedha za Mradi wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO -19 katika Mapori ya Akiba Swagaswaga na Mkungunero yanayopatikana katika Mikoa ya Dodoma na Manyara.

" Sisi ni Jeshi la Uhifadhi, na moja ya sifa ya msingi wa Jeshi lolote duniani ni kusimamia mambo makubwa mawili ambayo ni uadilifu na nidhamu," amesema Kamishna Wakulyamba.

Akizungumzia suala la uwepo wa wanyama wakali na waharibifu, Kamishna Wakulyamba amesema jukumu letu sisi kama wahifadhi ni kuendelea kudhibiti wanyamapori hawa ili wasilete madhara zaidi.

"Tuendelee kuweka mikakati madhubuti na tufanye kila linalowezekana kuhakikisha kuwa tunawadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu," Sisi ni Jeshi! Jeshi halishindwi. Tutimize wajibu wetu.

" Lakini nitumie nafasi hii kumshukuru kwa dhati kabisa Rais wetu kwa kuamua kuikuza sekta ya Utalii nchini na kuipatia Wizara ya Malisili na Utalii kiasi cha Shilingi bilioni 90 kupitia Mpango wa Ustawi wa Jamii na Mapambano dhidi ya UVIKO 10 ambapo TAWA ilipatiwa takriban bilioni 12.9 na leo tunashuhudia miundombinu ya kisasa ambayo imejengwa kupitia fedha hizo," aliongeza Kamishna Wakulyamba.

Aidha, Kamishna Wakulyamba alieleza kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya UVIKO 19 na kuipongeza Menejimenti ya TAWA kwa usimamizi mzuri wa miradi hiyo. Vilevile alielekeza Menejimenti kutangaza vivutio na fursa za uwekezaji vilivyopo katika Mapori hapo ili kuvutia wageni na wawekezaji wengi katika maeneo hayo.

Awali, akitoa salamu za ukaribisho kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi -TAWA, Kaimu Naibu Kamishna anayeshughulikia huduma za uhifadhi, Mlage Kabange alimshukuru Kamishna Wakulyamba kwa ujio wake na kumhakikishua kuwa maelekezo aliyoyatoa yatafika kwa watumishi wengine wa TAWA na hayataishia kwa watumishi wa Kanda ya kati pekee.

Kwa upande wake, Kamanda wa Uhifadhi, Kanda ya Kati, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Herman Nyanda alieleza kuwa jumla ya miradi Mitano imetekelezwa kupitia fedha za UVIKO -19 katika Mapori ya Akiba matatu yanayopatikana Kanda ya Kati ambapo katika Pori la Akiba Swagaswaga limejengwa lango la kisasa la kuingia wageni.

Kwa upande wa Pori la Akiba Mkungunero miradi iliyotekelezwa ni ujenzi wa geti la utalii, barabara yenye urefu wa kilometa 52 na eneo la kupumzika wageni  (picnic site).

Chapisha Maoni

0 Maoni