Hispania yazima ndoto za Uingereza kutwaa Kombe la Dunia

 

Timu ya taifa ya wanawake ya Hispania imeifunga Uingereza na kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia la Wanawake katika mchezo wa fainali uliochezwa Jijini Sydney nchini Australia.

Katika mchezo huo Hispania ilipata goli pekee kupitia kwa Kapteni Olga Carmona kwa kumpita kipa Mary Earps katika kipindi cha kwanza baada ya Lucy Bronze kupoteza mpira.

Kwa matokeo hayo Uingereza inaendelea kungojea kwa hamu kutwa Kombe la Dunia, baada ya Hispania kuwazidi mbinu.

Simba hao wakike walionekana kuwa watakuwa timu ya kwanza ya wakubwa ya Uingereza kutwaa ubingwa wa dunia, tangu timu ya wanaume kutwaa kombe la dunia mwaka 1966.

Wachezaji wa timu ya taifa ya wanawake ya Hispania wakishangilia kwa kuwa mabingwa wa dunia wa Kombe la Dunia la Wanawake 2023.

Chapisha Maoni

0 Maoni