Watoto ndio waliokuwa wa kwanza kulengwa kufunga hadi kufa
katika kutekeleza mahubiri ya siku za mwisho katika dhehebu la kanisa tata lililopo
Shakahola nchini Kenya, taarifa mpya zimeeleza.
Maelezo hayo mapya yametolewa wakati polisi wakiendelea na
uchunguzi na zoezi la ufukuaji wa makaburi ya watu wengi ambapo hadi sasa miili
200 imepatikana.
Aliyekuwa msaidizi wa muhubiri ameiambia New York Times kwamba
watoto waliuawa kwanza kwa kuamriwa kufunga wakiwa juani ili wafe haraka.
Msaidizi huyo Titus Katana amesema kwamba waliofuatiwa
kuagizwa kufunga hadi kufa ili wakutane na muokozi wao Yesu Kristo walikuwa ni
wanawake.
Katana ambaye anaisaidia polisi, ameeleza ukatili
waliofanyiwa watoto ukiwemo wa kufungiwa kwenye vipanda kwa siku tano bila chakula
wala maji.
Mchungaji Mkuu wa Kanisa hilo Paul Mackenzie mbali na kuwaagiza waumini wake wafunge hadi kufa alikuwa akiwahubiria wasiende shule wala wasiende hospitali.
Baadhi ya makaburi yaliyokwisha fukuliwa eneo la Shakahola na miili ya watu kutolewa na kuhifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
0 Maoni