Rukhsa sasa Ukraine kupewa ndege za kivita za F-16

 


Marekani imesema kwamba itawaruhusu washirika wake wa Magharibi kuipatia Ukraine ndege za kisasa za vita, zikiwamo zinazotengenezwa Marekani za F-16 ili kuisaidia uwezo wa kivita.

Mashauri wa Usalama wa Taifa wa Marekani Jake Sullivan, amsema Rais Joe Biden amewaeleza washirika wenzake wa G7 kuhusiana na uamuzi huo Ijumaa.

Vikosi vya Marekani pia vitawafundisha marubani wa Ukraine jinsi ya kutumia ndege zake, Bw. Sullivan amesema.

Ukraine iemekuwa ikiomba kupatiwa ndege za kivita zenye uwezo zaidi, Rais Volodymyr Zelensky amepongeza uamuzi huo na kusema kuwa ni wa kihistoria.

Kisheria, nchi zinaruhusiwa kuuza ama kusafirisha vifaa vya kivita vinavyotengenezwa na Marekani iwapo tu Marekani itaruhusu, hivyo rukhsa sasa ndege za F-16 kupelekwa Ukraine inayopigana na Urusi.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna serikali yoyote iliyothibitisha kwamba itaipatia Ukraine ndege hizo za kisasa.

Chapisha Maoni

0 Maoni