Mchezaji Jimmy Butler ameifungia Miami Heat pointi 27 wakati
wakiibwaga Boston Celtics kwa alama 111-105 na kuongoza ushindi wa 2-0 katika mfululizo
wa fainali za Eastern Conference
Butler alifunga pointi nane katika robo ya mwisho, huku wakiwa
nyuma kwa pointi 96-89, na kuparurana na Grant Williams wa Boston.
Katika mchezo huo Butler alipata rebounds sita, alisaidia
kupokonya mipira mara tatu, wakati Martin akifunga pointi 25.
0 Maoni