Hizi hapa timu nne zilizotinga nusu fainali CAFCC

 

Katika Droo ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho barani Africa (CAFCC) Yanga SC atakipiga na Marumo Gallants ya Afrika  ya kusini.

Mchezo wa kwanza katika hatua ya nusu fainali Yanga  wataanzia nyumbani Benjamin Mkapa mnamo Mei 10, 2023 na mchezo wa  marudiano utakuwa ni  huko Afrika Kusini Mei 17, 2023.


Wengine watakaokiputa kuingia fainali ni Asec Mimosas ya Ivory Coast wakikipiga na USM Alger.


Klabu ya Yanga ilitinga hatua ya nusu fainali kufuatia ushindi wa jumla wa 2-0 dhidi ya miamba ya Nigeria, Rivers United.


Huku Marumo Gallants ya  Afrika Kusini ikitinga kwa kuwachabanga  miamba ya Misri Pyramids kwa ushindi wa jumla wa 2-1.

Chapisha Maoni

0 Maoni