Mgombea
Udiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Nyandira, Ndugu Magari Nesto,
ameendeleza kunadi Ilani ya chama chake huku akisisitiza ushirikishaji wa
wananchi na serikali katika kupaisha maendeleo ya kata ya Nyandira.
Alitoa
kauli hiyo katika kampeni zake zinazoendelea katika kata hiyo wakati alipofanya
mkutano wenye mafanikio makubwa katika Kijiji cha Nyandira hapo jana, Oktoba 4,
2025.
Mkutano
huo, ambao mgombea huyo ameuelezea kuwa "mkutano bora kwa tarafa ya Mgeta
na Mlali tangu kuanza kwa kampeni," ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali
wakuu wa chama, akiwemo Mbunge mtarajiwa wa Wilaya ya Mvomero, Bi. Sara Msafiri
Ally, pamoja na viongozi wa kamati ya siasa ya Wilaya ya Mvomero, Mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya Mkoa, na Mjumbe mmoja kutoka Taifa.
Katika
mikutano yake yote aliyofanya tangu kuzindua kampeni, Ndugu Magari Nesto amesisitiza
ushirikishwaji wa wananchi na serikali katika kutatua matatizo yanayokabili
kata hiyo. Kampeni zake zimejikita katika kutembelea na kukutana na wananchi
katika vijiji vya Mwarazi (ambapo alizindua kampeni), Kibuko, na sasa Nyandira.
Katika
hotuba zake, mgombea huyo ametaja vipaumbele kadhaa vya kimaendeleo,ikiwamo
elimu, miundombinu, uchumi,masoko, utalii na mazingira.
Elimu:
Kuboresha utoaji elimu wenye ubora na kuimarisha mazingira bora ya shule za
msingi na sekondari.
Miundombinu:
Kushughulikia changamoto za mawasiliano, hasa katika uboreshaji wa miundombinu
ya barabara.
Uchumi na
Masoko: Kufanya juhudi za kuimarisha masoko ya bidhaa za wananchi wa Nyandira.
Utalii na
Mazingira: Kuendeleza uwezekano wa kuendesha utalii na kuhifadhi misitu kwa
ajili ya kurejesha hali ya hewa ya zamani.
Akizungumzia
mafanikio ya mikutano hiyo, hasa ule wa Nyandira, Ndugu Magari Nesto
aliwashukuru kwa dhati wananchi na viongozi wa Kata ya CCM kwa kujitoa kwao.
"Hakika
haikuwa rahisi kabisa kwasababu ya taratibu za Chama Chetu kwa jukumu la aina
hii kuandaliwa na Uongozi wa CCM kata, ambapo kwa 100% ninyi ndugu zangu kwa
michango yenu ndio imesaidia sana kufanyika vyema jambo hili kwa kiwango
hiki," alisema.
Alisema
kuwa rekodi ya mkutano huo na mingine ina maana kubwa sana kwao na kwa heshima
ya kata yao, akitarajia kupata ridhaa ya wananchi ili waanze kuwatumikia.
Mgombea Udiwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Nyandira,tarafa ya Mgeta mkoani Morogoro, Ndugu Magari Nesto , akiomba kura kwa staili ya aina yake wakati wa kampeni za kuomba ridhaa za wananchi kuwa diwani wa kata hiyo Oktoba 4, mwaka huu. (na Mpiga picha wetu).



0 Maoni