Rais Samia kuzindua leo DIRA ya Taifa ya 2050 Dodoma

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, atazindua rasmi Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 leo katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.

Dira hii ni mwongozo wa muda mrefu wa maendeleo ya taifa, unaolenga kuiongoza Tanzania kuelekea kuwa nchi yenye uchumi wa kati wa juu unaojali watu wake, mazingira na ustawi wa kijamii na kiuchumi ifikapo mwaka 2050.

Dira ya Maendeleo 2050 imejikita katika nguzo kuu kadhaa, ikiwemo:

·         Ukuaji wa uchumi jumuishi na shindani

·         Maendeleo ya watu na rasilimali watu

·         Utawala bora na utawala wa sheria

·         Uendelevu wa mazingira na rasilimali asilia

·         Matumizi ya teknolojia na ubunifu

Chapisha Maoni

0 Maoni