Mwenge wa Uhuru wazindua daraja la watembea kwa miguu la Tripri

 

Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndugu  Ismail Ali Ussi leo tarehe 16/7/2025  amezindua daraja la watembea kwa miguu katika kitongoji cha Tripri, Kata ya Gehandu,Halmashauri ya Mji wa Mbulu.

Ujenzi wa daraja hilo limesaidia kuondoa utoro kwa wanafunzi wa eneo hilo ambapo awali walishindwa kuhudhuria masomo hususan kipindi cha masika.

Aidha, daraja hilo limekuwa mkombozi kwa wakazi takribani 4,000 kwa kuwarahisishia usafiri na usafirishaji wa mazao.



Chapisha Maoni

0 Maoni