Mkutano Mkuu Maalum wa CCM kufanyika kwa njia ya mtandao kesho

 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeeleza kuwa kimekamilisha maandalizi ya mkutano mkuu maalumu wa chama hicho ngazi ya Taifa, unaotarajiwa kufanyika kesho, Julai 26, 2025, kwa njia ya mtandao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 25, 2025 jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Amos Makalla amesema kuwa maandalizi hayo yamefanyika kwa ufanisi katika ngazi zote za wilaya na mikoa nchini.

“Mkutano huu maalumu utafanyika kwa njia ya mtandao ili kurahisisha ushiriki wa wajumbe wote kutoka maeneo mbalimbali ya nchi,” alisema Makalla.

Ameeleza kuwa mkutano huo utaendeshwa kutokea jijini Dodoma na utatanguliwa na vikao vya Kamati Kuu pamoja na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Akifafanua kuhusu ajenda ya mkutano huo, Makalla amesema ajenda kuu itakuwa ni kujadili na kupitisha marekebisho madogo ya Katiba ya CCM.

Chapisha Maoni

0 Maoni