NHC yatekeleza kwa kasi mradi wa Samia Housing Scheme Dodoma

 

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Bw. Hamad Abdallah, ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za makazi katika eneo la Medeli, Jijini Dodoma, chini ya mradi wa Samia Housing Scheme.

Mradi huu unatekelezwa kwa kasi na umedhamiria kutoa makazi bora na ya kisasa kwa Watanzania, ikiwa ni sehemu ya mpango mkubwa wa ujenzi wa jumla ya nyumba 5,000 nchini. Tayari mpango huo umeanza kutekelezwa kwa mafanikio makubwa katika Jiji la Dar es Salaam, eneo la Kawe, ambako nyumba 560 zimejengwa.

Katika hatua nyingine ya utekelezaji, ujenzi wa nyumba za mradi huu umeanza pia katika eneo la Kijichi, Dar es Salaam.

Samia Housing Scheme ni mpango unaoenzi na kuendeleza maono ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha Watanzania wanapata makazi bora, salama na ya kisasa.

Kwa mara nyingine, Shirika la Nyumba la Taifa linaonesha dhamira ya dhati ya kutimiza wajibu wake wa kuwa msitari wa mbele katika sekta ya ujenzi wa nyumba za makazi, kwa ajili ya maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. 

                                       

#NHCTanzania #SamiaHousingScheme #Dodoma #MakaziBora #KaziInaendelea #TanzaniaInawezekana #UjenziWaMaendeleo

Chapisha Maoni

0 Maoni