TARURA yaweka jedwali la fidia ujenzi wa barabara Sindeni - Kwedukwazu

 

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Barabara Vijijini kwa Ushirikishaji wa Jamii na Ufunguaji wa Fursa za Kijamii na Kiuchumi (RISE) imefungua zoezi la kuweka wazi jedwali la fidia kwa wananchi watakaoathiriwa na mradi wa ujenzi wa barabara ya Sindeni - Kwedukwazu yenye urefu wa 38km inayotarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami katika kata ya Sindeni, wilayani Handeni mkoani Tanga.

Zoezi hilo linaratibiwa na kusimamiwa na wataalamu wa TARURA wakishirikiana  na Mhandisi Mshauri anaye "design" barabara hiyo ambapo lengo la zoezi hilo ni kuwapatia wananchi viwango vya fidia kwa maeneo yatakayopitiwa na Mradi baada ya maeneo yao kufanyiwa tathmini.

Barabara hiyo inatarajiwa kufungua na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii pamoja na kuunganisha vijiji vya Kweisasu, Mbuyuni, Kwankono, Komfungo, Komdudu, Sindeni na Sezakofi katika kata ya Sindeni, wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.



Chapisha Maoni

0 Maoni