Uvuvi wa vizimba chanzo muhimu cha uchumi Ziwa Victoria

 

Jitihada za ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba katika Ziwa Victoria zimeanza kuzaa matunda kufuatia wavuvi wa Musoma Vijijini Mkoani Mara kuvuna tani tani 12 za samaki wenye thamani ya fedha za Tanzania milioni 100.

Wavuvi hayo wamemweleza Mbunge wao wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo wamepata mavuno hayo ya idadi kubwa ya samaki kwenye kizimba kimoja chenye kipenyo cha mita 10 (10m-diameter).

Ufugaji huo wa samaki kwenye vizimba ni sehemu za jitihada za Prof. Muhongo za kuhakikisha wakazi wa Musoma vijijini wanaendelea kunufaika na Ziwa Victoria ambalo ndilo chanzo kikuu cha uchumi wa eneo hilo licha ya kuanza kuadimika kwa samaki.

Ziwa Victoria lina umri wa takribani miaka 400,000 na ujazo wake wa kawaida ni kilomita za ujazo 2,760 (2,760 cubic kilometres).

Mvua za mwaka jana ziliongeza ujazo wa maji ndani ya bonde la Ziwa Victoria lenye ukubwa kilomita za miraba 195,000 (195,000 square kilometres). Lilikuwa ongezeko la kina cha takribani mita 1.7 (ca. 1.7 meters depth).

Ziwa Victoria ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini:

Kata 18 kati ya Kata 21 za Jimbo letu zina ufukwe wa Ziwa Victoria. Kwa hiyo, asilimia 85.7 (85.7%) za Kata zetu zina fursa nzuri za kutumia raslimali za maji ya Ziwa hili.

Samaki wamepungua sana ndani ya Ziwa Victoria na mito inayolizunguka. Suluhisho la tatizo hili ni kuanzisha na kuendeleza uvuvi wa ufugaji wa samaki ziwani humo (aquaculture fish farming).

Upungufu wa samaki haupo tu ndani ya Ziwa Victoria, bali ni tatizo kubwa ulimwenguni kote! Bahari, maziwa na mito ya Duniani kote ina upungufu mkubwa wa samaki.

Kwa hiyo, kwa sasa takribani nusu (ca. 50%) ya samaki Duniani kote wanapatikana kupitia ufugaji wa samaki ndani ya bahari, maziwa, n.k. (aquaculture fish farming).

Uvuvi wa Vizimba Musoma Vijijini:

Malengo:

(i) Kata 18 kati ya 21 za Jimboni mwetu kuanzisha na kuendeleza Uvuvi wa Vizimba ndani ya Ziwa Victoria 

(ii) Mitaji ya Uvuvi wa Vizimba kupatikana kutoka:

(iia) Mitaji ya watu binafsi: vizimba 10 vimeishaanza uzalishaji

(iib) Mitaji kutoka mikopo nafuu ya Serikali Kuu: vizimba 8 tayari vimetayarishwa na kuwekwa Ziwani. Uzalishaji utaanza ndani ya miezi 3 ijayo

(iic) Mitaji kutoka mikopo mizuri ya Benki za Biashara (CRDB & NMB). Mikopo 10 ya vizimba 50 itatolewa hivi karibuni.

Mafanikio ya awali ya Uvuvi wa Vizimba:

Baadhi ya wavuvi wa vizimba wa Musoma Vijijini wamemueleza Mbunge wao wa Jimbo kwamba, kwenye kizimba kimoja chenye kipenyo cha mita 10 (10m-diameter) wamefanikiwa kuvuna tani 12 za samaki wenye thamani ya Tsh milioni 100 (Tsh 100m).

Chapisha Maoni

0 Maoni