Trump apingwa kwa kutaka kutwaa ukanda wa Gaza

 

Palestina, Misri na Saudi Arabia pamoja na mataifa mengine yamelaani kauli ya Rais Donald Trump, ya kupanga Marekani kuutwaa ukanda wa Gaza.

Trump amesema anataka Marekani kutwaa kwa muda mrefu mamlaka ya eneo hilo, na kulifanya kuwa eneo salama la Mashariki ya Kati.

Katika mpango wake huo Rais Trump amesema wakazi wake watahamishwa mbali na Gaza, ambapo viongozi wa Gaza wamesema hapana.

Hamas wamesema mipango hiyo ni “upuuzi”, huku Mamlaka ya Palestina ikisema Wapalestina hawatohamishwa, huku wakazi wa Gaza wakisema “hii ni ardhi yetu”.

Chapisha Maoni

0 Maoni