TFS yaibuka kinara wa udhamini yakabidhiwa tuzo

 

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dustan Kitandula, akimkabidhi tuzo ya kutambua mchango wa udhamini, Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo, kwa niaba ya Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango, wakati wa hafla ya kugawa zawadi kwa wadau waliofanikisha Kongamano la Tatu la Kimataifa la Kisayansi jana Disemba 11, 2024. Kongamano hilo linafanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 11-13 Desemba 2024 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

TFS imekuwa mmoja kati ya wadhamini wakuu wa kongamano hilo ili kuendeleza dhima ya uhifadhi wa misitu kwa maendeleo endelevu na kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi. Ushiriki wa TFS unalenga kuhamasisha tafiti za kisayansi zinazochangia kulinda mazingira, kuongeza uelewa wa jamii kuhusu uhifadhi, na kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali katika sekta ya misitu.

Chapisha Maoni

0 Maoni