Polisi wawili wauawa katika mapambano ya risasi

 

Askari polisi wawili wamepoteza maisha usiku wa kuamkia leo Desemba 18, 2024 kwa kushambuliwa kwa risasi na mtuhumiwa wa unyang'anyi wa kutumia silaha, Atanasio Malenda, wakati walipokwenda kumkamata nyumbani kwake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi amesema tukio hilo limetokea katika Kijiji cha Msagali wilayani Mpwapwa Mkoa wa Dodoma, ambapo pia Malendo (30) naye ameuawa.

Kamanda Katabazi, ameeleza kwamba tukio hilo limetokea saa 7 usiku wa kuamkia leo wakati askari D/Koplo Jairo Boniface Kalanda na Pc Alfred John walipokwenda kumkamata mtuhumiwa huyo.

Amesema askari hao waliuawa kwenye mapambano ya risasi na mtuhumiwa, akidaiwa alikuwa ametoka kumjeruhi Yohana Lameck na kumpora kiasi cha fedha shilingi milioni mbili.

Chapisha Maoni

0 Maoni