Bilionea Mulokozi anunua helkopta atua Manyara

 

Mkurugenzi wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited David Mulokozi amenunua Helkopta yake binafsi ambayo ametua nayo kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa Stadium akiwa ameambatana na familia yake.

Bilionea Mulokozi anaingia kwenye orodha ya miongoni mwa Watanzania wachache wanaomiliki ndege binafsi ambapo amesema kuwa kampuni yake imekua ikikua siku hadi siku na kuonyesha vitu vya tofauti.

“Hakuna mtu alitegemea kuwa Manyara kunaweza kuwa na helkopta ni mambo mengi yanaanza, wafanyabiashara wengi wanajifunza kila mtu anaruhusiwa kumiliki chombo hichi inawezekana,” ameeleza Mulokozi.

Mulokozi amesema kuwa helkopta hiyo itasaidia katika utoaji wa huduma katika kampuni yake inayojihusisha na uzalishaji wa vinywaji vyenye kileo na visivyo na kileo.

Pamoja na mambo mengine Bilionea Mulokozi ameiomba Serikali kujenga kiwanja cha ndege ili kuimarisha huduma za usafiri wa anga na ndege nyingi zaidi ziweze kutua mkoani Manyara.




Chapisha Maoni

0 Maoni