Papa Francis afichua jaribio la kutaka kumuua nchini Irak

 

Jaribio la kumuua Papa Francis wakati wa ziara yake nchini Irak, lilidhibitiwa baada ya watu wa Intelijensia wa Uingereza kutoa taarifa ya uwepo wa tukio hilo, kwa mujibu wa wasifu unaotarajiwa kutolewa.

Papa ameandika kuwa baada ya kutua kwa ndege Jijini Bhaghdad Machi 2021, aliambiwa kuwa hafla moja ambayo anatarajiwa kuwepo alikuwa ashambuliwe na watu wawili walioandaliwa kujitoa mhanga kwa mabomu.

Washambuliji wote wawili waliwahiwa kabla ya kutekeleza shambulizi hilo na kuuawa, Papa ameeleza katika sehemu ya taarifa hiyo, iliyochapishwa kwenye gazeti la nchini Italia la Corriere della Sera.

Ziara hiyo ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki duniani ilifanyika kwa siku tatu katika kipindi cha mlipuko wa virusi vya korona, ambayo ilishuhudiwa kuwapo kwa operesheni kali ya kiusalama.


Chapisha Maoni

0 Maoni