Dkt. Biteko asimulia alivyomfariji Mwananchi Mbagala

 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesimulia kisa cha mteja wa TANESCO Mbagala aliyefarijika baada ya kuelimishwa kuhusu Changamoto za upatikanaji wa umeme.

Dkt. Biteko ametoa simulizi hiyo Jijini Dar es Salaam hivi karibuni wakati akifungua Kongamano la Majadiliano ya Biashara na Uwekezaji kati ya Serikali na Sekta Binafsi Mwaka 2024 na Mkutano Mkuu wa 49 wa Mwaka 2024 wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA).

Dkt. Biteko amesimulia alivyoandikiwa meseji na mwananchi wa Mbagala, iliyosema, "Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, hivi mnatuoanaje ?, mnakata kata umeme tu mnavyojisikia mnakata kata tu umeme, sasa nina kwambia hivi kama mnafikiri kuwa hatukwaziki tunakwazika na Mungu atawalipa."

Ameeleza kuwa baada ya kupata ujumbe huo akajua kuwa mwananchi huyo amekasirika akamuambia pole ndugu yangu, leo tulitoa tangazo la kukata umeme kutokana na kazi ya kubadilisha transfoma ndogo na kuweka kubwa ambazo zitawafanya mpate umeme kwa uhakika.



Chapisha Maoni

0 Maoni