Burundi yafungua ubalozi mdogo Kigoma

 

Nchi ya Burundi imefungua ubalozi wake mdogo katika mkoani Kigoma nchini Tanzania ikiwa ni njia moja wapo ya jitihada za kuimarisha zaidi ushirikiano wa kiuchumi na kidiplomasia katika ya nchi hizo mbili.

Sherehe za ufunguzi zimehudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe.Thobias Andengenye na viongozi wengine mbali mbali kutoka Burundi akiwemo Katibu Mkuu wa chama kilichopo Madarakani cha CNDD FDD, Mhe. Reverien Ndikuriyo. Pia, wameadhimishwa miaka 20 ya ujirani mwema.

Pamoja na mambo mengine nchi hizi zimekubaliana kushirikiana katika kukomesha rushwa mipakani, biashara haramu ya binadamu na kuongeza muda wa nyaraka za ujirani mwema kutoka wiki mbili hadi miezi mitatu.

Mbali ya sherehe hizo, utachezwa mchezo kati ya Makamba Combine ya Burundi na Kigoma Combine katika uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma katika kunogesha ujirani mwema.

Chapisha Maoni

0 Maoni