Wafanyakazi wa Bunge la Marekani watembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti

 

Wizara ya Maliasili na Utalii imepokea Ujumbe wa Wafanyakazi wa Bunge la Marekani ukiongozwa na Bi. Courtney Butcher, ambao wamefanya ziara nchini kwa kutembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti kuanzia tarehe 26 hadi 28 Oktoba 2024.

Dhumuni la ziara hiyo ya miadi ni kujadili namna Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii zinavyokabiliana na shughuli za uwindaji haramu wa wanyamapori. Wageni hao wameelezwa na kuona kwa vitendo namna majangili wanavyotega mitego ya nyaya kwa ajili ya kupata wanyamapori na mitego hiyo inavyoteguliwa. Pia majadiliano yalifanyika kuhusiana na utalii, uhifadhi na changamoto zinazoikabili sekta ya utalii na uhifadhi nchini.

Taasisi za Wizara ya Maliasili ambazo zimeshiriki majadiliano hayo ni TANAPA, TAWA na NCAA.



Chapisha Maoni

0 Maoni