Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
(Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Ridhiwani Kikwete (Mb) ambae ni
Mgeni rasmi katika tukio la kupandisha Mwenge wa Uhuru katika kilele cha Mlima
Kilimanjaro tayari amewasili katika Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro na kulakiwa na
mwenyeji wake Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Balozi Pindi Chana (Mb).
Mhe. Ridhiwani ameongozana na Mkuu wa
Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi,
Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Zuhura Yunus na viongozi wengine waandamizi wa
serikali.
Zoezi la kupandisha Mwenge katika
kilele cha Uhuru linafanywa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ikiwa ni
sehemu ya sherehe za miaka 60 tangu kuanzishwa kwa mbio za mwenge huo.
0 Maoni