Rais Dkt. Mwinyi achangia milioni 100 ukarabati wa kanisa Zanzibar

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dkt Hussein Ally Mwinyi amechangia kiasi cha shilingi Milion 100 kwaajili ya ukarabati wa Kanisa katoliki la Minara Miwili lililopo Visiwani humo utakaogharimu kiasi cha shilingi Bilion 2.3.

Rais Dkt Mwinyi ametoa kiasi hicho  katika Tamasha la kumpongeza Askofu Agustino Shao wa Jimbo katoliki la  Zanzibar C.S.SP  Agustino Shao kwa kutimiza miaka 27 ya Uaskofu ambapo kanisa hilo lilijengwa zaidi ya miaka 125 iliyopita huku akisema  kuwa Serikali inalipongeza kanisa katoliki  hapa nchini kwa kuendelea kuhubiri amani, ushirikiano na mshikamano kwa watanzania wote.

Aidha Dkt Mwinyi ameahidi Serikali yake kuendelea kutoa ushirikiano kwa kanisa katoliki Visiwani humo pamoja na kutatua changamoto zote zinazozikabili taasisi za dini zilizopo.

Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Waziri wa nchi, ofisi ya waziri Mkuu sera, bunge na utaratibu  William Lukuvi amesema kuwa Rais Samia amechangia shilingi Milion 50 katika harambee hiyo.

Awali akizungumza Askofu wa Jimbo katoliki Zanzibar C.S.S.P. Agustino Shao amesema kanisa hilo ambalo ni miongozi mwa majengo ya kale yaliyopo Visiwani humo ni kivutio cha utalii kutokana na historia yake.

"Kanisa hilo ni kitomvu cha utalii linahitaji hadhi yake ili watu waone kwamba tunatunza historia yetu,  hasa wakati huu tunapotangaza uchumi wa blue tunaomba kanisa hilo liwe ni kitomvu cha utalii katika visiwa vyetu vya Zanzibar."

Mbali na wananchi waliohudhuria harambee hiyo iliyofanyika katika uwanja wa Mau  Chama Cha ACT Wazalendo Zanzibar kimeahifi kuchangia kias cha Shilingi Million 5.

Na. Denis Chambi- Zanzibar



Chapisha Maoni

0 Maoni