Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 27, 2024 amehudhuria katika Tamasha la Buhaya ‘Buhaya Festival’ linalofanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Lengo la tamasha hilo ambalo mgeni
rasmi ni Waziri Mkuu Majaliwa ni kutangaza na kutambulisha fursa za vivutio vya
utalii na uwekezaji vinavyopatikana mkoani Kagera.
Aidha, Tamasha hilo pia linalotoa
fursa ya kuenzi na kuendeleza mila na desturi za jamii ya Wahaya kutoka ndani
na nje ya Mkoa wa Kagera.
0 Maoni