Rapa Sean “Diddy” Combs anakabiliwa na
tuhuma mpya za ubakaji, udhalilishaji wa kingono na shambulizi la ngono, baada
ya mfululizo wa mashtaka mapya kufunguliwa jumatatu.
Karibu mashtaka sita yamefunguliwa
dhidi rapa huyo maarufu kama P Diddy katika Mahakama ya Shirikisho New York na
wanawake wawili na wanaume wanne. Tuhuma hizo zinaanzia mwaka 1995 hadi 2021.
Washtaki ambao hawajatajwa majina yao
wamesema baadhi ya mashambulizi ya kingono yalifanywa kwenye sherehe za Combs,
ambazo zilihudhuriwa na watu maarufu na wanamuziki.
Wanasheria wa Combs, wamekanusha
tuhuma hizo, na katika taarifa yao kwa vyombo vya habari wamesema mteja wao
hajawahi kufanyashambulizi la ngono kwa mtu yeyote mzima, mtoto, mwanaume ama
mwanamke.
0 Maoni