Mchezaji nyota wa mpira wa kikapu wa
Marekani LeBron James (39) ameweka historia katika Ligi ya NBA kwa kucheza
mchezo akiwa timu moja na mwanaye Bronny James (20).
Bonny James aliingia katika robo ya
pili ya mchezo huo wa mechi za awali za msimu za Ligi ya NBA ambao Los Angeles Lakers walilala kwa vikapu 118-114 dhidi ya Phoenix Suns.
Haijawahi kutokea katika Ligi ya NBA
ya Marekani kwa mtoto kucheza mchezo na baba yake, katika hatua zozote zile za
michezo ya ligi hiyo ikiwamo ya michezo ya awali ya msimu.
0 Maoni