Kimbunga Milton kimeikumba jimbo la Florida
nchini Marekani kikisababisha mafuriko na kutishia kuongezeka kwa gharika.
Nyumba zaidi ya milioni moja na maeneo
ya biashara yamekosa umeme na kuna taarifa za kutokea vifo katika Pwani ya
Atlantic.
Huko St Perersburg, pwani ya magharibi
ya jimbo hilo, paa la uwanja wa ligi ya mpira wa baseball limepasuka kwa upepo
mkali.
Kimbunga Milton kilichokuwa na kipimo
cha daraja la tano, kimeshushwa daraja hadi kufika la kwanza, hata hivyo bado
kina madhara.
0 Maoni