Tufanye kazi, siasa haitoleta mkate mezani- Dkt. Biteko

 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuwagawa na badala yake kuungana na kushirikiana ili kuchochea maendeleo na ustawi kiuchumi na kijamii huku akisema siasa haitoleta mkate mezani isipokuwa kufanya kazi.

Dkt. Biteko ameyasema hayo wakati akihutubia mkutano wa hadhara Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma.

 "Siasa haitoleta mkate mezani isipokuwa kufanya kazi, hata tukija Wanasiasa hapa tukawaambia kunja na ngumi, baada ya kukunja ngumi hautokuja mkate mezani, lazima Watu wafanye kazi, tunaweza kutumia siasa kwa Watu na maisha yao tukazungumza chuki zetu dhidi ya Watu, kutugawanya, kugawanya Nchi hii, tunazo Nchi ambazo Watu walianza kidogokidogo kugawanyika, baadaye wakaishia kwenye kupigana, tutanye siasa za kutuleta pamoja," alisema Dkt. Biteko.

Chapisha Maoni

0 Maoni