Wanafunzi wapatao 17 wamekufa baada ya shule yao kuungua moto nchini Kenya usiku wa Alhamisi, polisi wa nchi hiyo wamesema.
Inahofiwa kuwa idadi ya vifo ikaongezaka kutokana na
wanafunzi wengine zaidi kupelekwa hospitali wakiwa wameungua vibaya.
Chanzo cha moto huo katika shule hiyo ya msingi ya Hillside
Endarasha iliyopo kaunti ya Nyeri bado kinachunguzwa, Msemaji wa Polisi Resila
Onyango amesema.
Onyango amesema timu ya wachunguzi imeshafika shuleni hapo kwa ajili ya kuanza uchunguzi wa tukio hilo la moto.
0 Maoni