Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inawaomba wataalam wa
afya kutoka Hospitali za Wilaya, Mikoa na Rufaa nchini kuwatuma wagonjwa wenye
matatizo ya kuziba kwa mishipa ya damu ili watibiwe katika kambi maalum ya
uchunguzi na matibabu ya kuzibua mishipa hiyo.
Matibabu hayo yatakayotolewa tarehe 22 hadi 28 Septemba 2024
yatafanywa na wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Andalusia
ya nchini Misri.
Matibabu yatakayotolewa katika kambi hiyo ni ya kuzibua
mishipa ya damu ya artery iliyoziba kwa kutumia mtambo wa Cathlab, upasuaji kwa
njia ya kutumia matundu madogo katika kutibu mishipa ya damu ya vein
iliyotanuka kwa kutumia kifaa cha umeme kijulikanacho kwa jina la laser
ablation, kuzibua mishipa ya damu (veins) ya shingo iliyoziba (ballooning) kwa
kutumia mtambo wa Cathlab hasa kwa wagonjwa wa dialysis wanaotumia catheter
kwaajili dialysis.
Aidha tunawaomba wagonjwa wenye matatizo ya ganzi miguuni, vidonda vya miguu visivyopona kwa muda mrefu, matatizo ya mishipa ya damu miguuni.
0 Maoni