Bondwa Hiking Club, Polisi waipa moto kauli ya Waziri Mkuu

 

KLABU ya mazoezi ya Bondwa Hiking ya Mkoani Morogoro kwa kushirikiana na jeshi la polisi Mkoani humo limefanya matembezi ya Kms 15 na mbio za Hisani Kms 30 lengo likiwa ni kuunga mkono wito wa waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa la kuwata wananchi kushiriki mazoezi ya ili kuweza kupambana na magonjwa mbalimbali yasio ambukiza.

Mbio hizo ziliongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda Ya Morogoro Mhe. Latifa Mansoor kwa kushirikiana na maafisa askari wa jeshi la Polisi, watumishi wa Mahakama pamoja na baadhi ya joking club  zilizopo mkoani humo.

Aidha, katika mbio hizo kuligawanyika kundi jingine ambalo lilotembea umbali wa Km 15 kuzunguka maeneo tofauti ya Ndani ya Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza wakati wa kuhitimisha mbio na matembezi hayo Jaji wa Mahakama Kuu kanda ya Morogoro Latifa Mansoor aliipongeza Club ya Bondwa Hiking Club pamoja na jeshi la polisi kwa kuweza kushirikiana katika kuandaa tukio hilo hali ambayo limesaidia kuimarisha afya ya mwili pamoja na akili.

 Hata hivyo Mhe Latifa Mansoor amesema kuwa Klabu hiyo imewapa hamasa na wao kama Mahakama sasa watakuwa wakishirikiana na Jeshi la polisi Kila Jumamosi ya Mwisho wa mwezi katika kufanya mazoezi ya pamoja.

Akimuwakilisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Afisa mnadhimu wa jeshi la polisi Mkoani humo ACP Yohana Mjengi amesema kuwa jeshi hilo litaendelea kufanya maoezi ya pamoja kila mwisho wa mwezi ili kuimarisha afya zao.

Aidha amepongeza ushirikiano ulionyeshwa na Klabu ya Bondwa katika maandalizi hadi kufanyika kwa mbio pamoja na matembezi hayo ambayo yalikuwa na lengo kuunga kwa vitendo kauli mbiu ya waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambayo ailiitoa mapema mwezi huu.

Kwa upande wake Wakili Mwansoho ambae ni mwenyekiti wa Club ya Bondwa hiking amesema kuwa licha ya wao kujiunga kwa pamoja katika kufanya mazoezi ili kupambana magonjwa yasiyo ambukizwa pia wamekuwa wakihamasisha utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji.

Sanjari na hilo ameeleza kuwa klabu hiyo imekuwa akitoa misaada mbalimbali kwa watu wasiojiweza na wenye mahitaji maalumu.

Nae Mratibu wa Club hiyo George Matiku amesema kuwa takribani askari zaidi ya 90 wa Kikosi cha Kutuliza Ghasi waliweza kushiriki mbio za km 30 huku Zaidi ya Askari 120 wakishiriki katika matembezi ya KMs15 huku Makamu Mwenyekiti Juma Mbonde akieleza kuwa tangu kuanza hadi kumalizika kwa matembezi na mbio hizo hakuna aliyepa majeraha yeyote hivyo wote waliweza kumaliza salama.

Katika zoezi hilo kijana mwenye Umri wa miaka 12 wa Darasa la Sita  Ally Silim Seif aliweza kumaliza mbio za Kms 30 ambapo amewataka watoto wenzie kujikita katika kufanya mazoezi kwani pia inasaidia kuimarisha uwezo wa kufikiri hasa katika masomo yao.



Chapisha Maoni

0 Maoni