Diwani wa kata ya Bujora wilayani Magu, Mwanza Bunyanya John,
ametoa msaada wa baiskeli 54 kwa wanafunzi wa kike katika shule ya Sekondari
Lumve ili kuwapunguzia adha ya kutembea umbali mrefu kwenda shule.
Akikabidhi baiskeli hizo diwani huyo amesema wanafunzi hao
wamekuwa wakipata changamoto mbalimbali zikiwemo za kuvamiwa na wanayama wakali
pindi wanapoenda shule huku wengine wakikatisha masomo hivyo baiskeli hizo
zitasaidia kuwaondolea changamoto hizo.
“Baiskeli mlizopata leo naomba mzitumie vizuri katika
kurahisisha usafiri wa kutoka nyumbani kuja shule ili muweze kuongeza ufaulu
maana njiani mlikuwa mnapata chanagmoto nyingi kama kuvamiwa na wanyama wakali,
wengine hupata vishawishi na kuishia kukatisha masomo wengine kufanyiwa vitendo
vya ukatili, sasa mkazitumie vizuri baiskeli hizi.”
Kwa upande wao wanafunzi Hellen Mmasi na Esther John
wameshukuru kupata msaada wa baiskeli hizo na kuahidi kufanya vizuro katika
masomo yao.
“Baiskeli hizi zitatusaidia kwa kiasi kikubwa kuepuka
changamoto kwani tutawahi shuleni na kufaulu kwa kufanya vyema kwenye masomo
yetu kwani tutawahi shule na kupata muda mzuri wa kujisomea,” wamesema
wanafunzi hao.
Mdau wa maendeleo aliyeshirikiana na Diwani wa kata hiyo ya
Bujora Jefta Kishosha akatoa wito kwa wazazi kuwa mstari wa mbele kuwasaidia
watoto wao katika utunzaji wa baiskeli hizo na kuacha kuzitumia kwa matumizi
tofauti na yaliyokusudiwa ikiwemo na kubeba mizigo na maji.
0 Maoni