Serikali kupitia Wizara ya Afya imesitisha kampeni ya umezeshaji
wa kinga tiba za ugonjwa wa mabusha na matende katika Halmashauri ya Jijini la
Da es Salaam, Manispaa ya Temeke na Kata 10 za Manispaa ya Kinondoni ambazo hazina
maambukizi mapya ya ugonjwa huo.
Waziri wa Afya Mhe. Ummy
Mwalimu amesema hayo jana Machi 12, 2024, wakati akiongea na wandishi wa habari
juu ya hatua zilizofikiwa za kutokomeza ugonjwa wa mabusha na matende nchini hususan
katika Mkoa wa Dar es Salaam.
“Serikali kwa kushirikiana na wadau tumeweza kudhibiti ugonjwa
huu katika Halmashauri 112 kati ya 119 na kubakiwa na Halmashauri 7 ambapo mafanikio
hayo yamechangiwa na kampeni za utoaji elimu na umezaji kinga tibaza ugonjwa huo zilizofanyika katika maeneo mbalimbali yanchi,”
amesema Waziri Ummy.
Aidha, Waziri Ummy amesema bado kuna baadhi ya Halmashauri ambazo
bado zina maambukizi mapya ya ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na Pangani, Mafia,
Kinondoni, Kilwa, Lindi Manispaa, Mtamana Mtwara Mikindani ambapo kwa ujumla
kata hizo zinawakazi 1,203,359.
"Natoa rai kwa wakazi wa maeneo hayoa mbayo bado kuna maambukizi
ya ugonjwa huu kujitokeza kwa wingi ili kushiriki kwenye kampeni za kinga tiba ya
ugonjwa wa matende na mabusha zitakazoendelea kufanyika katika maeneo yao ilikuweza
kutokomeza maambukizi mapya ya ugojwa huu," amesema Waziri Ummy.
Amesema, Kigamboni na Ubungo hazina maambukizi mapya kwa kipindi
cha miaka sita baada ya kusitisha umezaji wa kingatiba huzo hatua iliyowezesha watu
milioni 3.7 kuokolewa katika hatari ya kupata maambukizi mapya jijini Dar es
Salaam.
Waziri Ummy amemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan kwa kuendelea kujali afya zaWatanzania ambapo amewezesha upatikanaji wa fedha
pamoja na vifaa katika kufikia mafanikio hayo.
Kwa upande wake, Mratibu Udhibitiwa Ugonjwa wa Matende na Mabusha
Wizara ya Afya, Dkt. Faraja Lyamuya amesema sababu zinazochangia maambukizi mapya
katika baadhi ya maeneo ni jamii kutokuwa na uelewa wakutosha pamoja nak uhamahama
hali inayosababisha kutoshirikiki kamilifu katika umezaji wa kinga tiba.
Kuhusu maambukizi mapya kuwepo katika maeneo ya Pwani zaidi amesema
ni kwa sababu ya hali ya hewa na mazingira ambayo huruhusu mazalia ya mbu na kwamba
maeneo ya mazalia yenye mbu wengi ndiyo yalionekana kuwa na kiwango cha juu cha
maambukizi.
Tathmini inaonyesha kambi ya mwisho ya upasuaji wa mabusha na
matende ilifanyika mwaka 2023 na kuvu kalengo la kufanya upasuaji kwa zaidi yawatu
1,100.
0 Maoni