Jamii
ya Kabila la Wairaq wanaoishi mikoa ya Arusha na Manyara mwishoni mwa
wiki iliyopita walifanya sherehe kubwa ikiwemo dua na sala maalum na
kukemea laana iliyofanywa na wazee wao karne kadhaa zilizopita za
kuwaua watoto wa kike waliopata ujauzito nje ya ndoa.
Tukio
hilo kubwa lilifanyika jumamosi iliyopita katika makumbusho ya Urithi
Geopark mjini Karatu na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali
wakiongozwa na naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Daniel Sillo na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Frederick
Sumaye.
Viongozi wa kutoka kabila hilo walipongeza jitihada
kubwa zinazofanywa na watoto wa kike ambao kwa miaka sasa wamekuwa na
maendeleo makubwa kiuchumi, kielimu na kisiasa na kusisitiza umuhimu
wa kuendelea kuwaendeleza wanawake ambao wana mchango mkubwa katika
maendeleo ya Taifa.
Naibu spika wa Bunge Mhe. Sillo aliwataka
wananchi wa kabila hilo kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ili
kujiletea maendeleo sambamba na kulinda amani ya taifa.
Tukio
hilo lilitanguliwa na ibada kubwa pamoja na mambo mengine kukemea
laana iliyofanywa na Kabila hilo miaka kadhaa iliyopita ya kuua
watoto wa kike waliopata ujauzito nje ya ndoa na kueleza kuwa laana
ya kuwaua watoto wa kike waliopata ujauzito nje ya ndoa itaendelea
kukemewa ili laana hiyo isiendelee kuumiza maisha ya kizazi cha sasa
na kijacho cha kabila la Wairaqw.
Tukio hilo lililofanyika
Makumbusho ya Urithi Geopark Karatu ni kuenzi historia na utamaduni
wa makabila mbalimbali yanayounda Geopark ya Ngorongoro Lengai ambapo
historia yao
imetunzwa katika makumbusho hiyo.

.jpeg)


0 Maoni