EU yatenga milioni 400 kukabiliana na kipindupindu

 

Katika kukabiliana na mlipuko wa kipindupindu nchini Tanzania, Umoja wa Ulaya (EU) umetenga kiasi cha Euro 150,000 sawa na shilingi milioni 414 za Tanzania kwa ajili ya misaada ya kibinadamu.

Msaada huo wa Umoja wa Ulaya unalenga katika kuisaidia Tanzania kuudhibiti mlipuko wa kipindupindu, ambao unahatariasha maisha ya watu milioni 4 katika mikoa iliyokumbwa na  ugonjwa huo.

Taarifa iliyotolewa leo Machi 4, 2024 na Umoja wa Ulaya imesema mlipuko wa kipindupindu unazidi kushika kasi kwenye mikoa 13 ya Tanzania, ambayo ilipatwa na ugonjwa huo tangu Januari 2024.

Takwimu zinaonyesha kuwa watu 1,500 wameugua ugonjwa huo wa kipindupindu ambapo miongoni mwao 34 wamefariki dunia. Msaada huo wa EU utatumika kwa miezi mitatu hadi mwishoni mwa Mei 2024.

Chapisha Maoni

0 Maoni