Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amepokea salamu
za pole kutoka kwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa Mhe.Balozi Dkt.Emmanuel Nchimbi
akiongozana na wajumbe baadhi wa Sekretarieti ya Halmashauri ya Chama cha
Mapinduzi Taifa waliofika Ikulu Zanzibar jana.
Wajumbe hao akiwemo
Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar Dkt.
Mohamed Dimwa, Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Paul Makonda,
Katibu wa NEC Idara ya Organaizesheni Ndugu Issa Haji Ussi (Gavu), Katibu wa
NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndugu Rabia Abdallah Hamid kufuatia kifo cha Baba yake Mzazi, Mwenyekiti
wa CCM Taifa Mstaafu, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyefariki dunia tarehe: 29 Februari 2024,
Dar es Salaam na kuzikwa tarehe: 02 Machi 2024, Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini
Unguja.
0 Maoni