Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki
amewataka Watanzania kufungua Makumbusho zao binafsi kwa mujibu wa Sheria ili
historia na kumbukumbu muhimu ziweze kubakia kwa manufaa ya vizazi vya sasa na
vijavyo.
Mhe.Kairuki ametoa kauli hiyo katika Kituo cha wakati
akifungua onesho kuhusu Mahusiano baina ya Tanzania na India katika kituo cha
Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam shughuli iliyoendana
sambamba na Maadhimisho ya Miaka 75 ya Uhuru wa Taifa la India.
"Ziko taratibu wakija hapa Makumbusho wataelekezwa, kuna ambao watataka
kuanzisha makumbusho ya ukoo, makumbusho za taasisi, tunawakaribisha nyote
mpate miongozo ili muweze kufanikisha ndoto na azma yenu."
Kwa upande wake Naibu balozi wa India nchini Tanzania, Mhe.
Manoj Varma ameomba Taasisi ya Makumbusho ya Taifa kulifanya onesho hilo kuwa
la kudumu kwa kuzingatia mahusiano ya muda mrefu ya mataifa hayo tangu Karne ya
19 kwenye nyanja za kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa la Tanzania, Dkt.Noel Lwoga amesema ufunguzi wa onesho hili ni mwanzo wa kuanzishwa kwa Makumbusho binafsi ya Taifa la India itakayokua hapa nchini ili kuendelea kurithisha historia ya mahusiano baina ya mataifa haya mawili kwa vizazi vijavyo.
0 Maoni