Rais Samia atembelea Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Januari Makamba, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo pamoja na viongozi wengine wakifuatilia wasilisho la historia ya Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma nchini Indonesia wakati akihitimisha ziara yake nchini humo tarehe 26 Januari, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha Karafuu cha Indesso, Robby Gunawan kuhusu mchoro maalum unaoashiria mchakato mzima wa utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na Karafuu nchini Indonesia tarehe 26 Januari, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo kuhusu kazi mbalimbali zinazofanyika katika Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma wakati akihitimisha ziara yake nchini Indonesia tarehe 26 Januari, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa katika Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma nchini Indonesia wakati alipohitimisha ziara yake tarehe 26 Januari, 2024. Kiwanda hicho kikubwa kinatengeneza bidhaa mbalimbali kutokana na malighafi ya zao hilo la Karafuu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo kuhusu kazi mbalimbali zinazofanywa katika Kiwanda cha Karafuu cha Indesso Aroma nchini Indonesia wakati alipohitimisha ziara yake tarehe 26 Januari, 2024. Kiwanda hicho kikubwa kinatengeneza bidhaa mbalimbali kutokana na malighafi ya zao hilo la Karafuu.

Chapisha Maoni

0 Maoni