Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete
anesema eneo la ununuzi wa umma limekuwa likiripotiwa kugubikwa na
vitendo vya rushwa na ubadhirifu ambapo
zaidi ya asilimia 72 ya bajeti ya Serikali imekuwa ikitumika kwenye
manunuzi hayo ya umma.
Amesema kutokana na
uzito huo Serikali kupitia
Mamlaka ya Serikali Mtandao imeamua kusanifu, kujenga na kusanikisha Mfumo wa
Kitaifa wa Kielektroniki wa Ununuzi Tanzania {National e-Procurement System of
Tanzania (NeST)} ili kuweza kukabiliana na changamoto hiyo.
Mhe. Kikwete ametoa kauli hiyo leo Jijini Arush wakati
akifunga kongamano la 14 la mwaka la wataalam wa ununuzi na
ugavi zaidi ya 900 lenye kauli mbiu "Mabadiliko ya kidijitali kwa ajili ya
kuboresha usimamizi na ugavi kelekea maendeleo endelevu".
Amesema mfumo huo utasaidia kuondoa mianya ya rushwa na upendeleo na hivyo thamani ya pesa za Serikali katika bidhaa na huduma italindwa kwani kutakuwa hakuna ulazima wa watu kukutana ana kwa ana.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.Ridhiwani Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watendaji mara baada ya kuwasili kufunga kongamano la 14 la mwaka la wa ununuzi na ugavi uliofanyika Jijini Arusha
0 Maoni