Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amewataka waganga wakuu wa Hospitali za Rufaa za Mikoa na Wilaya kuboresha utoaji wa huduma katika hospitali zao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwakua Serikali haitamvumilia kiongozi yoyote anayekwamisha juhudi za uboreshaji wa huduma katika sekta ya afya nchini.
Dkt. Molel ametoa kauli hiyo
leo alipofanya ziara katika Hoaspitali ya Taifa Muhimbili kuangalia hali ya
utoaji huduma na kufanya mazungumzo na Wakuu wa Taasisi za Afya ikiwemo MNH,
JKCI, MOI, MSD, NHIF, TMDA, Mganga Mkuu wa mkoa pamoja na Waganga Wafawidhi wa
Hospitali za Rufaa za mkoa wa Dar es Salaam
Akizungumza katika kikao
hicho, Naibu Waziri wa Afya ameeleza kuwa mafanikio katika uboreshaji wa huduma
sio uwekezaji wa vifaa tiba na rasilimali watu pekee bali ni pamoja na kuwepo
kwa uongozi bora na kila mmoja kutimiza wajibu wake.
‘’Mh. Rais wa Awamu ya Sita
Dkt.Samia Suluhu Hassan ameshamaliza kazi yake kwa kuwekeza Trilioni 6.7 katika
miundombinu, taaluma, teknolojia tiba na rasilimali watu sasa ni wakati wa kila
kiongozi kutekeleza majukumu yake kwakua sera ya Wizara ya Afya kwasasa ni
kuhakikisha Hospitali za Serikali zinatoa huduma bora zinazokidhi viwango’’
amesema Dkt. Mollel.
‘’Mh. Waziri wa Afya Ummy
Mwalimu ameniagiza kutembelea hospitali zote nchini kuangalia suala la ubora
katika utoaji huduma na kufanya marekebisho katika maeneo ambayo hayafanyi
vizuri, kiongozi kama hutekelezi majukumu yako inavyotakiwa unapaswa
kujitafakari, hata hivyo napenda kuzipongeza Taasisi za MNH, MOI na JKCI kwa
kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya ‘’amesisitiza Dkt. Mollel.
Wakati huohuo Dkt. Mollel
amesema Wizara ya Afya imedhamiria kuhakikisha kuwa mifumo ya TEHAMA katika
hospitali kuanzia ngazi ya zahanati hadi taifa inasomana ili kumpunguzia muda
mgonjwa wa kusubiri kupata matibabu kwa kurudia kufanya kipimo isipokua pale
inapolazimu kurudia kufanya kipimo husika.
0 Maoni