Msemaji wa Mashirika ya
Umoja wa Mataifa, ameeleza kuwa kumekuwapo na matukio ya vifo kwa pande zote
mbili za Gaza na Isarel, na kusema kwa wastani watoto 160 wanauawa kila siku
Gaza.
Mapema Shirika la Afya
Duniani (WHO) lilisema kiwango cha matukio ya vifo na mateso katika vita hiyo baina
ya Israel na Hamas ni vigumu kuingia akilini.
Wakati huo huo Waziri wa
Ulinzi wa Israel Yoav Gallant amesema vikosi vya nchi hiyo vipo katika maeneo
ya kati ya Mji wa Gaza.
Gallant amesema vikosi vya
Israel vimeingia katika mji huo kutokea kaskazini na kusini kwa ushirikiano wa
vikosi vya aridhini, anga na majini.
0 Maoni