Mwanaume mmoja amekufa kwa
kuminywa na roboti Korea Kusini, baada ya roboti kushindwa kumtofautisha mtu
huyo na maboksi ya chakula iliyokuwa ikiyabeba.
Tukio hilo limetokea wakati
mwanaume huyo mwenye miaka 40, muajiriwa wa kampuni inayotumia roboti alipokuwa
akikagua utendaji kazi wa roboti.
Mkono wa roboti
ulijichanganya na kudhani mtumishi huyo ni boksi la mbogamboga, na ilimnyanyua
na kumkandamiza kwenye mkanda unaozunguka na kumpasua kichwa na kifua.
Mwanaume huyo alikimbizwa
hospitali lakini taarifa za shirika la habari la Korea Kusini la Yonhap
zimesema alifariki akiwa hospitali.
Kwa mujibu wa Yonhap, roboti
hiyo ilikuwa inahusika katika kunyanyua maboksi ya karatasi na kuyapondaponda hadi
kuyafanya kuwa punje punje.
0 Maoni