Polisi nchini Kenya wamewaachia huru watu watatu waliowakamata
kwa kushiriki maandamano ya kuiunga mkono Palestina, katika Jiji la Nairobi.
Waandamanaji hao wameachiwa huru Jumapili bila ya
kufunguliwa mashtaka, baada ya Serikali kukosolewa mno na wanasiasa pamoja na
makundi ya haki za binadamu.
Mbunge wa Kenya Yusuf Hassan alishutumu kitendo cha
kukamatwa waandamanaji hao.
Mkuu wa Amnesty International nchini Kenya, Irungu Houghton
amesema kuvuruga maandamano hayo ni kinyume cha sheria na ni kitendo cha kusikitisha
mno.
Rais wa Kenya William Ruto alielezea msimamo wa Serikali
yake wa kuiunga mkono kikamilifu Israel katika vita vinavyoendelea.
0 Maoni