Mashambulizi ya anga ya usiku mzima katika ukanda wa Gaza
yamesababisha idadi kubwa ya vifo na majeruhi kwa mujibu wa taarifa ya Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Palestina.
Wizara hiyo imeposti taarifa yake kupitia Telegram, ikisema
kwamba mashambulizi hayo ya anga ni ya usiku wa jana na leo asubuhi.
Wizara pia imetoa picha ambazo zinaonyesha milipuko kwenye
majengo na watoa huduma za dharura wakifukua miili ya watu kwenye vifusi baada
mashambulzi.
0 Maoni