Urudishaji mikopo ya elimu kwa hiyari bado ni tatizo- HESLB

 

Licha ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini (HESLB), kuwawezesha mikopo wanafunzi zaidi ya 750,000 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2004, bado inakabiliwa na tatizo la urejeshaji mikopo kwa hiyari.

Mkurugenzi Mkuu wa bodi hiyo, Bw. Abdul-Razaq Badru ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam katika mkutano wake na Wahariri wa Vyombo vya Habari, chini ya uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.

“Bodi ya mikopo ipo katika hatua ya kuunganisha mfumo wake na taasisi zingine za Serikali ikiwemo wa Hifadhi za Jamii na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ili kuhakikisha inawapata wale wote waliokopa kwenye bodi hiyo,” amesema Bw. Badru

Kuhusu makusanyo ya mikopo, Bw. Badru amesema hadi kufikia Septemba 2023, fedha zilizokusanywa na HESLB kutoka kwa wakopaji zaidi ya 230,000 zinakadiriwa kufika Tsh. 1.3 trilioni.

Akizungumzia wanufaika wa mikopo Bw. Badru amesema katika mwaka 2023/24 kuna jumla ya wanufaika 229,652 wa mikopo wanaochukua shahada, Samia Scholarship na Diploma, waliotengewa kiasi cha shilingi bilioni 786.

Chapisha Maoni

0 Maoni