NIC yainadi bima ya nyumba kujikinga na El Nino

 

Kufuatia Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA) kutabiri uwepo wa mvua kubwa za mvua za vuli zitazokuwa na El Nino kuanzia katika mwezi huu wa Oktoba hadi Desemba, Shirika la Bima (NIC) limewashauri wananchi kukatia bima za nyumba zao ili kuzikinga na madhara yanayoweza kusababishwa na mvua hizo.

TMA walitoa tahadhari ya uwepo wa mvua ya El Nino inayotokana na mabadiliko ya tabia nchi na kusema maeneo ya Pwani ya Kaskazini na ukanda wa Ziwa Victoria yataathiriwa na mvua hizo, kwa kutambua umuhimu wa wakazi wa maeneo hayo NIC imewashauri kukata bima ya nyumba zao ili pindi yakitokea madhara waweze kulipwa na kuepuka kukosa makazi.

“Bima ya nyumba ni bima ambayo inalinda mmiliki wa nyumba endapo nyumba yake inaweza kupata madhara yasiyodhurika mfano mafuriko au imeungua moto wote tunasikiliza vyombo vya habari tumesikia kwamba kuna mvua kubwa inategemewa kunyesha kwahiyo sisi kama NIC tunatoa wito kwa watu wakate bima za nyumba kwa ajili ya kukinga nyumba zao endapo mvua kubwa itanyesha na kuleta madhara kama mafuriko basi wasipate hasara na kuanza kuilalamikia Serikali kuomba msaada wa nyumba zao kukumbwa na mafuriko wakate bima itayosaidia kuwalipa na kujenga nyumba zao,” amesema Stella Marwa Meneja wa NIC Kanda ya Ziwa.

Chapisha Maoni

0 Maoni