Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi amesema nchi imeandika historia mpya kwa kuwakabidhi vyeti
vya uraia wa Tanzania wahamiaji wasiohamishika 3,319 ambao wameishi nchini kwa
zaidi ya miaka 50 wakiwa na asili ya mataifa jirani ya Burundi, Comoro,
Msumbiji na Rwanda.
Rais Dk. Mwinyi amesema hayo leo tarehe 05 Septemba 2023
katika hafla ya kukabidhi vyeti vya uraia wa Tanzania kundi la Wahamiaji
wasiohamishika Ikulu, Zanzibar.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi amefurahishwa kutekelezwa ahadi yake
aliyoitoa baada ya kuingia madarakani mwaka 2020 kwa kumalizika zoezi hilo na
kuwafanya watambulike kuwa Raia wa Tanzania badala ya Wahamiaji wasiohamishika.
Vilevile, Rais Dk. Mwinyi ametoa wito kwa Idara ya Uhamiaji
nchini kuziimarisha sheria zilizopo hususani sheria ya uraia wa Tanzania kwa
kuwa sheria hii haijafanyiwa mapitio kwa kipindi kirefu kwa madhumuni ya
kuiwezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowahusu wananchi na wageni
wanaofika nchini.
🗓️05 Septemba, 2023
0 Maoni